Habari Mpya

Friday 31 October 2014

kutoka kwa tiba na chakula leo ebu jifunze kitu hapa,Tumia tiba asilia kukuza/kujaza nywele zako.


Kitunguu maji ‘Onion’: Kata vipande vidogovidogo vya vitunguu maji weka kwenye shampuu yako acha vikae kwa muda wa siku 15 kisha tumia shampoo yako, si kwamba itasaidia kukuza nywele zako tu bali itasaidia kuzifanya nywele zako zingae na ziwe na afya.
Mdarasini, Kitunguu maji chekundu,karafuu na kitunguu swaumu
Kata kitunguu maji chukundu nusu changanya na karafuu tatu, kitunguu swaumu na miti miwili ya mdarasini. Weka kila kitu kwenye sufuria chemsha kwa muda wa dakika 15. Ukishafanya hivyo acha mchanganyiko wako upoe kisha uoshe nywele zako kila siku kwa siku nne.
 
Mafuta mbegu za zabibu ‘Grape seed oil’
Mafuta ya zabibu yanaaminika kwenye kukuza nywele, tumia mafuta hayo kupaka kwenye ngozi chini ya nywele kisha fanya masaji kabla ya kupana kitanda, ukihitaji mafuta haya nitafute.
Vidonge vya kuzuia mimba ‘Birth Control Pills’
Saga vidonge vya kuzuia mimba changanya na shampoo yako. ukiosha tumia hiyo iliyochanganywa utaona matokeo, mbali na kukuza pia inazifanya zinajaa na kukomaa.
Aloe Vera na asali ‘honey’
Kata majani matatu ya aloe vera toa ute wake changanya na asali kisha paka chini ya ngozi acha kwa muda wa dakika 20 kisha safisha.
Maji ya rozi ‘Rosemary water’
Akila siku pakaa maji ya rozi kwenye nyele zako hasa eneo la chini ya ngozi.
Maji ya viazi -Potato water
Kama utakuwa unapika viazi chukua maji ya viazi yaliyopata moto osha nywele zako, yanasaidia kukuza nywele.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: kutoka kwa tiba na chakula leo ebu jifunze kitu hapa,Tumia tiba asilia kukuza/kujaza nywele zako. Description: Rating: 5 Reviewed By: fashion time na tatyana celestine
Scroll to Top