Juisi ina faida nyingi katika mwili wa binadamu, zipo juisi za aina
mbalimbali ambazo zinatokana na mimea na mizizi aliyoumba Mwenyezi
Mungu.
Juisi ya Tende ni miongoni mwa juisi zilizojizolea umaarufu mkubwa hasa katika kurekebisha tatizo la nguvu za kiume.
MAHITAJI :
Tende kilo moja
Maziwa ya unga au ya ng’ombe lita moja
Sukari kiasi upendacho.
KUMBUKA : Tende zina asili ya sukari hivyo hakikisha unaweka kiasi kidogo.
NAMNA YA KUTENGENEZA :
Chukua tende zako kisha zitoe mbegu zake.
Hakikisha unatoa mbegu tu na kuziacha tende kama zilivyo bila kutoa kitu kingine.
Anza kuzisaga peke yake kwenye brenda hadi zitakapolainika sawasawa.
Mimina maziwa yako kidogokidogo kwenye brenda ili kuzisaga vema jambo litakalosaidia juisi yako kulainika vema.
Baada ya kutia maziwa yote na kuisaga sawasawa, tia sukari kiasi
upendacho huku ukiendelea kuisaga ili sukari yako iweze kuchanganyika
vizuri na juisi yako.
Juisi yako itakuwa tayari kwa kunywa sambamba na kitafunwa chochote ukipendacho kama vile bagia, sambusa, korosho au karanga.
Warembo kutoka nchi mbali mbali walioingia fainali za Miss Grande Internationale mwaka jana. Picha na Maktaba
Kwa mara ya kwanza katika historia, mshiriki kutoka Tanzania
ataliwakilisha Taifa kwenye mashindano ya urembo ya kimataifa
yanayofahamika kama ‘Miss Grand International 2014 (MGI) yatakayofanyika
mwishoni mwa mwaka huu Bangkok, Thailand.
Shindano
hilo litajumuisha warembo kutoka zaidi ya nchi 70 duniani, litatoa fursa
kwa kila mmoja kuonyesha umahiri wake katika kuwakilisha tamaduni za
nchi zao hasa katika mavazi.
Akizungumza na gazeti hili
Mkurugenzi wa Miss Grand International Tanzania, Veronika Rovegno,
alisema timu yake imejipanga kuhakikisha Tanzania inanyakua taji hilo.
“Tanzania
itashiriki kwa mara ya kwanza, lakini hiyo si sababu ya kuwa
wasindikizaji. Tumejipanga na tutahakikisha mshiriki wetu anakwenda
Thailand kushindana na siyo kufanya majaribio,” alisema
Vero
aliwataka warembo kuendelea kutuma maombi yao kwa wingi wakizingatia
vigezo vyote vilivyotolewa katika tovuti ya Miss Grand International.
Hii itarahisisha katika zoezi la kufanya uchaguzi wa mwanzo kabla ya kufanyika kwa onyesho hilo nchini.
“Hivi
sasa tupo kwenye mchakato wa kupokea majina na sifa za washiriki
zilizoambatanishwa na picha zao, baadaye tutafanya mchujo wa mwanzo
kabla la shindano lenyewe,” alisema Vero.
Mwaka jana
mrembo, Janelee Chaparro kutoka Puerto Rico aliibuka mshindi na
kuwabwaga washiriki wenzake wapatao 70. Katika mashindano hayo Bara la
Afrika liliwakilishwa na nchi za Algeria, Misri, Ethiopia, Kenya, Uganda
na Zimbabwe.
0 comments:
Post a Comment