Habari Mpya

Wednesday 27 December 2017

BASATA YAKANUSHA TAARIFA ZA LINO AGENCY

Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) limekanusha taarifa iliyotolewa na waandaaji wa shindano la Miss Tanzania ya LINO Agency, kwamba Baraza hilo ni moja ya chanzo cha kukwamisha shindano hilo kufanyika.

PICHA NA MTANDAO
Kweye taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari, BASATA imesema ilitoa kibali cha muda kwa kampuni hiyo kuweza kushughulikia matatizo yake, pamoja na kuratibu safari ya Miss Tanzania 2017 aliyeshiriki mashindano ya Miss World mwaka huu.
Taarifa hiyo imeendelea kwa kutoa wito kwa makampuni yanayoandaa mashindano ya sanaa kuongeza weledi, na kuzingatia sheria, ili kuepuka matatizo kama hayo.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: BASATA YAKANUSHA TAARIFA ZA LINO AGENCY Description: Rating: 5 Reviewed By: fashion time na tatyana celestine
Scroll to Top