Habari Mpya

Sunday 31 August 2014

UKISTAAJABU YA MUSSA UTAONA YA........ mwanamke mwenye rasta ndefu ajabu

Asha Mandela (47) kutoka Atlanta, Georgia amefuga nywele hizo kwa miaka 25. Inasemekana zina urefu wa futi 55. Asha amegoma kuzikata nywele zake licha ya kushauriwa na madaktari kutokana na madhara ya kupooza ambayo anaweza kuyapata. Alisema nywele hizo zimekua kama sehemu ya mwili wake, ni maisha yake hivyo kamwe hawezi kuzikata.
Asha huzichukulia nywele hizo kama mtoto wake. Humchukua siku mbili kuziosha na kuzikausha nywele hizo.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: UKISTAAJABU YA MUSSA UTAONA YA........ mwanamke mwenye rasta ndefu ajabu Description: Rating: 5 Reviewed By: fashion time na tatyana celestine
Scroll to Top