Habari Mpya

Thursday 2 January 2014

Usijinyime kula ili kupungua uzito

YAPO maswali mengi kuhusu tatizo la ukubwa wa matumbo yetu hasa kwa sisi  wanawake.
Wengi wamekuwa wakitumia njia mbalimbali ambazo nyingine si sahihi sana katika kufanya ili mradi kuwemo na amani akilimi na kwenye mwili.
 
Wengi wetu tunataka matumbo yawe wastani hasa yale ambayo hayajitokezi katika nguo zetu.
Ipo njia ya haraka ya kupunguza tumbo njia hiyo ni kubadili mfumo wa ulaji.
Unaweza kwa kuanza kula mbogamboga na matunda kwa wingi na kupunguza kula vyakula vya kukaanga na kufanya mazoezi ya kutembea.
Njia salama ya kupunguza tumbo ni ile ya kupangilia vyakula, usijinyime kula kwa kudhani kwa kufanya hivyo unaweza kupunguza tumbo njia hiyo inaweza kuleta madhara makubwa . Punguza kula vyakula vyenye wanga tumia mboga mboga na matunda kwa wingi pia punguza vyakula vyenye sukari nyingi.
Vyakula kama viazi mviringo, wali, mkate hukaa tumboni zaidi ya siku tatu, Unashauriwa kuacha kula nyama nyekundu ambayo husababisha kuongeza uzito na kuongezeka kwa ukubwa wa tumbo pia.
Unaweza kuwa unakula vizuri na unafanya mazoezi lakini ukawa na tatizo hili, kuna wakati tumbo linajitokeza kuliko kawaida. Mara nyingi hali hii husababishwa na kula vyakula vya wanga kwa wingi kama hunywi maji ya kutosha, kula bila mpangilio maalum au kula mara moja kwa siku.
Kula milo mitatu kwa siku .Kunywa maji mengi  angalau lita tatu kwa siku sababu kubwa ya mtu kuwa na tumbo kubwa ni chakula anachokula.
 




 
 
 
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Item Reviewed: Usijinyime kula ili kupungua uzito Description: Rating: 5 Reviewed By: fashion time na tatyana celestine
Scroll to Top